Mwanzo > Habari > Content

Mwalimu Mkuu wa BFSU Atembelea Hong Kong, Macao na Zhuhai

Updated: 2026-04-26

Tarehe 21-26 Aprili, Mwalimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Jia Wenjian ametembelea Hong Kong, Macao na Zhuhai.

Wajumbe wa BFSU wamehudhuria Kongamano la Elimu ya Juu la Vyuo Vikuu vya Asia; kutembelea Chuo Kikuu cha Mji cha Hong Kong, Shirika la Upatanisho la Kimataifa (IOMed), Baraza la Kutunga Sheria la Macao , Chuo Kikuu cha Macao, Mfuko wa Macao, Taasisi ya Macao ya Chuo Kikuu cha Umoja wa Mataifa, Chuo Kikuu cha Ufundi Anuwai cha Macao, Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Macao, Ofisi ya Serikali ya China mjini Macao, Chuo cha Ubunifu wa Mashariki na Magharibi cha Macau, Kituo cha Huduma za Uchumi na Biashara kati ya China na Nchi Zinazozungumza Kireno na Kihispania; kujadiliana kuhusu miradi mbalimbali, ikiwemo Mkutano wa Vijana wa Asia-Pasifiki wa Kuigiza Umoja wa Mataifa wa 2026; kuwatembelea wahitimu wa zamani wa BFSU; na kuimarisha ushirikiano na taasisi husika katika nyanja za mashirika ya kimataifa, kutayarisha wasomi, ufundishaji, utafiti, uchapishaji wa pamoja, mawasiliano ya kitaaluma, n.k. Jia Wenjian na viongozi wa taasisi husika wametia saini makubaliano ya ushirikiano.


Baidu
map