Tarehe 11 hadi 14 Mei, Mkuu wa BFSU Prof. Jia Wenjia ametembelea Urusi. Wajumbe wa BFSU wametembelea Chuo Kikuu cha Lugha cha Moscow, Chuo Kikuu cha Lomonosov, Chuo Kikuu cha Urafiki wa Wananchi cha Urusi, Chuo Kikuu cha Sanaa cha Urusi, Chuo Kikuu cha Saint Petersburg, na Taasisi ya Maandishi ya Mashariki iliyo chini ya Taasisi ya Sayansi ya Urusi. Pia wametembelea Ubalozi wa China nchini Urusi na Ubalozi Mdogo wa China mjini Saint Petersburg, kutembelea Delo Group, na kuanzisha Jumuiya ya Wahitimu wa BFSU nchini Urusi.
